Cholemu architecture ni dawati lililoanzishwa na kampuni ya Cholemu investment ltd inayojihusisha na uuzaji wa viwanja na mashamba kwa mikopo isiyo na riba wala dhamana.
Dawati hili lilianzishwa baada ya kugundua kuwa wateja wengi wanakutana na changamoto za ujenzi baada ya kupata viwanja vyao. Kwa maana hiyo dawati hili lipo mahususi kwa kusaidi wateja wa cholemu investment na watanzania wote kwa ujumla wanaohitaji ushauri katika masuala ya ujenzi.
Dawati letu lina wataalamu mbalimbalia wa masuala ya ujenzi wakiwemo wasanifu majengo na wakandarasi.
Kupitia tovuti yetu hii utaweza kuona baadhi ya ramani zetu za majengo mbalimbali na kuzipakua bila gharama yoyote.
Ni vizuri kufuata ushauri kwa wataalamu wa ujenzi kabla ya kuanza ujenzi wa nyumba/jengo ili kuepukana gharama zisizo za lazima.
Tunachora ramani za nyumba na majengo mbalimbali.
Tunatoa huduma ya ujenzi kwa wateja wenye ramani zao.
Tuanakarabati nyumba na majengo yaliyochakaa ama kubomoka.
Tunafanya makadirio ya gharama za ujenzi.
Tunatoa ushauri kuhusu masuala ya ujenzi kwa kuzingatia Ubora, Viwango na gharama.
Tunatoa huduma za usimamizi wa ujenzi kuanzia hatua za mwanzo (design) mpaka mwisho (finishing).
Fungua ukurasa wetu uliondika "RAMANI" au bofya hapo chini "RAMANI" kisha uchague na kupakua ramani utakayo. Baada ya hapo tupigie simu na ututajie namba ya ramani utakayo (Mfano A1, A3, B2) kisha utapata mchanganuo wake na gharama yake.
2019 | Design by PUSH DIGITAL